Wednesday 31 January 2018

SANAA NI KAZI

#EastAfricaArtBiennale

"Sanaa ni kazi kama ilivyo kazi nyingine, tuna kila sababu ya kuilinda, kuithamin na kuiendeleza sanaa hii ya uchoraji. 


Nimeona hapa kuna picha zina bei kubwa sana, lakini bei hii haimzuii mteja kuinunua kazi hii, kwani thamani na ubora wa kazi husika ndio unaofanya bei kuwa kubwa au ndogo.


Ndugu wasanii, Tanzania ya viwanda inakuja na muda si mrefu wachoraji wataanza kuhitajika kwa wingi zaidi kwenye viwanda kwenda kuchora viatu, magauni nk.

Lakini pia mbali na kutuinua kiuchumi, sanaa inatuunganisha kijamii watu wa tamaduni mbalimbali na mataifa mbalimbali leo tupo hapa kwa ajili ya sanaa hii.

Kama serikali tunapata fursa na mialiko mbalimbali kuhusu sanaa hii, hivyo nawashauri ndugu zangu wasanii tuje tujisajili Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) ili tutambuane na tupate takwimu sahihi miongoni mwetu na hatimaye tuweze kugawana fursa hizi kiurahisi mara tu zinapojitokeza." Kaimu Katibu Mtendaji wa BASATA Bw. Onesmo Kayanda. (Tarehe 06/11/2017 kwenye ukumbi wa Alliance Française - Dar es Salaam)







 

No comments:

Post a Comment