Wednesday 31 January 2018

MH. WAZIRI AKUTANA NA WASANII

Picha na Dondoo za tukio la Waziri mwenye dhamana na Sanaa Dkt. Harrison Mwakyembe na Naibu wake Juliana Shonza walipokutana na Wasanii wa Fani zote tarehe 27/10/2017 kupitia programu yetu ya Jukwaa La Sanaa. Katika kikao hicho waziri ametolea majibu kero zifuatazo:

1. Suala la muda wa Wasanii wa Muziki katika maenesho yao ambapo kumekuwa na kubanwa muda na kulazimishwa kukatisha maonesho. Waziri amesema tayari ameshazungumza na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda na tayari kamati imeundwa kupitia sheria ndogo za manispaa zinazokwamisha.

2. Sheria ya hakimiliki na maboresho yake yako katika hatua za mwisho na ameeleza kwamba ni nzuri na itatatua matatizo ya wizi wa kazi za Wasanii.

3. Kuundwa kwa Idara za Sanaa katika halmashauri. Ameeleza ameshazungumza na Waziri mwenye dhamana na TAMISEMI kuhusu suala hili na linafanyiwa kazi. Ameahidi kulitolea ripoti.

4. Amezungumzia wasanii kutokaa kimya wanapodhulumiwa haki zao. 
Amewataka kuanza kutumia TEHAMA katika kuuza kazi zao 
na kuepuka watu wa kati ambao wamekua wakifaidika zaidi yao. Ameeleza kufurahishwa na Shirikisho la Sanaa za Ufundi ambalo tayari limezindua mfumo wa TEHAMA katika kunadi na kuwafaidisha wasanii wa Sanaa za Ufundi.







No comments:

Post a Comment