Tuesday 26 September 2017

WASANII WANUFAIKA NA ELIMU YA BIASHARA KWA NJIA YA MITANDAO KUTOKA BASATA

Katibu mtendaji wa Baraza Bw.Godfrey Mngereza upande wa kulia akisubiri kufungua semina, pembeni yake ni wataalamu wa masuala ya mitandao Bw.Sarehe Juma na Michael Mlingwa kutoka kituo cha utangazaji cha Clouds Media Group waliokuwa wanatoa mafunzo hayo.

Katika kukuza na kuendeleza sekta ya Sanaa hapa nchini, kama ilivyo ada Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) limeendesha semina ya kuwajengea uwezo wasanii wa kuitumia kibiashara mitandao ya kijamii "social medias". Semina hiyo ilifanyika katika ukumbi wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) kwa siku tatu kuanzia tarehe 29 hadi tarehe 31 Agosti 2017 na wadau mbalimbali wa Sanaa wapatao sitini (60) walihudhuria semina hiyo.

Semina hiyo iliendeshwa na BASATA kwa kushirikiana na wataalamu wa masuala ya kimtandao kutoka kituo cha Utangazaji cha Clouds Media Group ambao ni Bw. Michael Mlingwa na Bw. Salehe Juma. Aidha wataalam hawa walianza kwa kufafanua maana ya mitandao ya kijamii lakini pia walieleza aina mbalimbali ya mitandao ya kijamii ambayo mfano Twiter, Instagram, Facebook, Imo, You Tube nk.

Walifundisha namna ya kufungua/kutengeneza akaunti katika mitandao hii na kuitumia katika kutafuta marafiki kwa lengo la kutaka kupashana habari na kufanya nao biashara mitandaoni walisema.. 

msanii anaweza chonga kinyago na kukipiga picha akatupia mtandaoni na wakaona watu wengi zaidi tena ndani ya muda mchache tu”.


Mitandao hii inasaidia sana katika kutafuta masoko ya kazi za wasanii mitandaoni kiurahisi na kwa haraka na kuwafikia watu wengi zaidi. 

Aidha wataalamu hao walifundisha namna ya kufanya biashara mtandaoni, walisema.
msanii anaweza kufungua akaunti ya Instagram mfano watu maarufu kama akina Diamond, Alikiba nk wanatumiwa na makampuni kutangaza biashara zao na kujitengenezea pesa kupitia majina yao


Na mwisho mgeni rasimi kutoka BASATA ambaye alialikwa kuja kuhitimisha semina hiyo Bi. Nsao Vivian Shalua aliwataka wasanii kutumia elimu waliyoipata katika kazi zao ili kuendana na mabadiliko ya sayansi na tekinolojia na alisema 

tumepanga kukuza sanaa kwa kuwazungukia wasanii huko walipo ili kuwapatia elimu itakayo wasidia katika kazi zao za kisanaa na kuwapa nafasi ya kulijua baraza la Sanaa la Taifa (BASATA)”.

Lakini pia wasanii wote walioudhuria semina hiyo walitambuliwa na BASATA kwa kupewa vyetu vya kuhitimu. 

No comments:

Post a Comment