Wednesday 13 September 2017

LILIAN LOTH KUIWAKILISHA TANZANIA MASHINDANO YA MISS AFRICA CONTINENTAL 2016/2O17



Katibu mtendaji wa Baraza La Sanaa La Taifa (BASATA) Bw.Godifrey Mngereza (aliyevaa miwani) akimkabidhi bendera ya Tanzania mshiriki wa mashindano ya Miss Africa Continental (Lilian Loth) yanayo tarajiwa kufanyika nchini Afrika ya kusini (Johannesburg). Makabidhiano hayo yalifanyika ofisini kwake Jijini Dar Es salaam.



Mwanadada  Lilian Loth Lazaro mshindi wa  mashindano ya Miss Tanzania Continental 2016/2017 amekabidhiwa rasmi bendera ili kuiwakilisha Tanzania katika mashindano ya Miss Africa continental yanayotarajiwa kufanyika  Afrika ya kusini (johannesberg) mwaka huu. Makabidhiano hayo yalifanyika katika ofisi ya katibu mtendaji wa Baraza La Sanaa La Taifa(BASATA) 22/08/2017.


Lilian Loth alikabidhiwa bendera hiyo baada ya kushinda mashindano ya Miss Tanzania Continental yanayofanyika kila mwaka yakiwa na lengo la kutafuta mshindi atakaye iwakilisha Tanzania katika mashindano ya Miss Africa continental. Mashindano hayo hujumuisha washindi mbali mabali wanao wakilisha nchi zao, yaani kila nchi hutoa mshindi mmoja ili ashiriki mashindano hayo na mwisho kumpata mmoja atakaye wakilisha Afrika katika mashindano ya Dunia.


Mashindao hayo yalianzishwa tokea mwaka 2014,  na hii imekuwa mara ya kwanza Tanzania kutoa mshiriki katika mashindao haya. Mashindano haya huusisha mwaafrika yeyote mwenye vigezo vya kutosha kuitambulisha vyema Afrika katika kueneza utamaduni, mila na desturi za kiafrika.

Mwanadada Lilian Loth Lazaro mwenye umri wa miaka 22 akitokea chuo kikuu cha kampala university anayesoma shahada ya utawala amekuwa mshiriki wa kwanza kushiriki mashindano haya hapa nchini baada ya kushinda mashindano ya Miss Tanzania Continental yaliyofanyika mwaka huu hapa Tanzania.


Aidha katibu mtendaji wa Baraza La Sanaa La Taifa (BASATA) Bw.Godifrey Mngereza alimkabidhi bendera hiyo na kumtaka aiwakilishe vyema Tanzania katika mashindano hayo na alisema ‘nenda ukaiwakilishe  vizuri Tanzania na sisi watanzania tupo nyuma yako na Mungu akubariki’

Mshiriki wa mashindano ya Miss Africa Continental Lilian Loth akiwa na Katibu mtendaji wa Baraza La Sanaa La Taifa Bw. Godifrey Mngereza mara baada ya kukabidhiwa rasmi bendera ya Tanzania ili kuiwakilisha Tanzania katika mashindano hayo Afrika kusini mwaka huu.



No comments:

Post a Comment