Tuesday 12 September 2017

WASANII JIUNGENI NA MFUKO WA HIFADHI YA JAMII.


Bw. Magira Werema (Afisa mikopo kutoka mfuko wa hifadhi ya  jamii (PSPF) akitoa elimu juu ya kujiunga na PSPF kwa wasanii katika viwanja vya Baraza La Sanaa La Taifa (BASATA) alipokuwa kwenye Jukwaa la Sanaa



"Wasanii wengi hapa nchini bado hawajajiunga na mifuko ya hifadhi ya jamii", hayo yalisemwa  na  Bw. Magira Werema (Afisa Mikopo kutoka  Mfuko wa hifadhi ya jamii PSPF)  tarehe 21 Agosti 2017 alipokuwa  kwenye Jukwaa la Sanaa katika viwanja vya Baraza La Sanaa La Taifa (BASATA) ambapo jumla ya wadau  wapatao  sabini (70) walihudhuria programu  hiyo.

Bw. Magira Werema  Afisa mikopo kutoka mfuko wa hifadhi ya jamii (PSPF) aliwataka  wasanii  kujiunga na mfuko wa PSPF ili waweze kunufaika na huduma zinazotolewa na mfuko huo kwani  PSPF wamelenga kusaidia katika majanga  yasiyo kingika kama Magonjwa, Ajari pamoja na Ulemavu. Bw. Werema alisema  “wasanii wengi wanahangaika hasa wanapopatwa na magonjwa hali ambayo huwalazimu kuomba msaada kutoka serikalini
au kuchangishana wao kwa wao ili waweze kupata matibabu”  ilikuondokana na usumbufu huo akawaomba  wasanii wajiunge na PSPF.
Bali na hayo, pia Bw. Magira alieleza mafao mbalimbali yanayotolewa na PSPF mafao hayo ni Fao la Elimu na Ujasilia mali, Mafao ya bima ya afya, Fao la uzeeni, Mikopo ya nyumba pamoja  na viwanja, pia  fao la ulemavu linatolewa, hivyo basi wanachama wake wananufaika na mafao hayo.

Hivyo basi aliwataka wasanii wajiunge  na PSPF ili wanufaike na mafao hayo, kwani wasanii wengi wanahangaika hasa baada ya kuzeeka na hii husababishwa na ukweli kuwa, muziki una muda wake na hufikia kipindi cha kupumzika hivyo basi wakiwa na PSPF wanaweza kupatiwa fao la uzeeni na kuwasaidia kama wasitaafu wengine wanavyo nufaika na mafao ya uzeeni.     
  
Katika Jukwaa hilo, Bw. Augustino Makame kutoka  Baraza La Sanaa La Taifa (BASATA) alitowa ombi kwa PSPF kutafuta namna ya kuwafikia wasanii  hasa waliopo mikoani kwani PSPF haipo kwa  ajiri ya wasanii wa Dar es  salaam tu, pia aliomba PSPF  wawatumie wasanii katika kazi zao hasa wanapokuwa wanahamasisha watu kujiunga na mfuko huo   na wafanyapo mikutano ili kuwainua wasanii.













Na mwisho Bw. Magira alitowa wito kwa wasanii kujiunga na PSPF kwani wakati ni sasa na haina haja kubaki wakihangaika, na alisema hakuna gharama ya kujiunga na mfuko huo, wadau pamoja nawasanii waliokuwepo kwenye Jukwaa hilo waliitikia wito huo kwakuchukua fomu za kujiunga na mfukohuo kwa wingi,  kwani elimuiliyotolewa ilionekana kuwahamasisha kujiunga na mfuko huo.
Bw.Magira Werema (afisa mikopo kutoka PSPF) akijibu maswali mbalimbali kutoka kwa wadau ikiwa ni pamoja na kuelekeza hatua za kujiunga na mfuko huo, ambapo alisema hakuna ghalama yoyote ile inayotozwa ili kujiunga na PSPF
Bw. Magira Werema mwenye suti nyeusi akiwa na Bw. Augustino Makame kutoka ( BASATA) wakijaribu kuchambua changamoto mbalimbali kutoka kwa wadau waliokuwepo kwenye Jukwaa hilo.
Mmoja wa wadau wa sanaa aliyekuwepo kwenye Jukwaa hilo akiuliza swali kwa muwezeshaji hasa juu ya faida  za kujiunga na mfuko wa hifadhi ya jamii PSPF  na hatutua za kujiunga na mfuko huo.

Wadau mbalimbali wa sanaa wakifuatilia kwa makini hoja mbalimbali zilizokuwa zikitolewa katika mkutano huo.

No comments:

Post a Comment