Tuesday 26 September 2017

MH. DKT. WAZIRI MWAKYEMBE ATOLEA UFAFANUZI .

Mh. Waziri Dkt.Harrison Mwakyembe akanusha vikali kuagiza kufutwa kwa mashindano ya Urembo 
(Miss Tanzania) na Tuzo za Muziki. Atoa ufafanuzi kuhusu kauli yake aliyoitoa hivi karibuni wakati akihojiwa na kituo kimoja cha radio kuhusu matukio haya muhimu kwa sekta ya Sanaa na Burudani nchini.



WASANII WANUFAIKA NA ELIMU YA BIASHARA KWA NJIA YA MITANDAO KUTOKA BASATA

Katibu mtendaji wa Baraza Bw.Godfrey Mngereza upande wa kulia akisubiri kufungua semina, pembeni yake ni wataalamu wa masuala ya mitandao Bw.Sarehe Juma na Michael Mlingwa kutoka kituo cha utangazaji cha Clouds Media Group waliokuwa wanatoa mafunzo hayo.

Katika kukuza na kuendeleza sekta ya Sanaa hapa nchini, kama ilivyo ada Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) limeendesha semina ya kuwajengea uwezo wasanii wa kuitumia kibiashara mitandao ya kijamii "social medias". Semina hiyo ilifanyika katika ukumbi wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) kwa siku tatu kuanzia tarehe 29 hadi tarehe 31 Agosti 2017 na wadau mbalimbali wa Sanaa wapatao sitini (60) walihudhuria semina hiyo.

Semina hiyo iliendeshwa na BASATA kwa kushirikiana na wataalamu wa masuala ya kimtandao kutoka kituo cha Utangazaji cha Clouds Media Group ambao ni Bw. Michael Mlingwa na Bw. Salehe Juma. Aidha wataalam hawa walianza kwa kufafanua maana ya mitandao ya kijamii lakini pia walieleza aina mbalimbali ya mitandao ya kijamii ambayo mfano Twiter, Instagram, Facebook, Imo, You Tube nk.

Walifundisha namna ya kufungua/kutengeneza akaunti katika mitandao hii na kuitumia katika kutafuta marafiki kwa lengo la kutaka kupashana habari na kufanya nao biashara mitandaoni walisema.. 

msanii anaweza chonga kinyago na kukipiga picha akatupia mtandaoni na wakaona watu wengi zaidi tena ndani ya muda mchache tu”.


Mitandao hii inasaidia sana katika kutafuta masoko ya kazi za wasanii mitandaoni kiurahisi na kwa haraka na kuwafikia watu wengi zaidi. 

Aidha wataalamu hao walifundisha namna ya kufanya biashara mtandaoni, walisema.
msanii anaweza kufungua akaunti ya Instagram mfano watu maarufu kama akina Diamond, Alikiba nk wanatumiwa na makampuni kutangaza biashara zao na kujitengenezea pesa kupitia majina yao


Na mwisho mgeni rasimi kutoka BASATA ambaye alialikwa kuja kuhitimisha semina hiyo Bi. Nsao Vivian Shalua aliwataka wasanii kutumia elimu waliyoipata katika kazi zao ili kuendana na mabadiliko ya sayansi na tekinolojia na alisema 

tumepanga kukuza sanaa kwa kuwazungukia wasanii huko walipo ili kuwapatia elimu itakayo wasidia katika kazi zao za kisanaa na kuwapa nafasi ya kulijua baraza la Sanaa la Taifa (BASATA)”.

Lakini pia wasanii wote walioudhuria semina hiyo walitambuliwa na BASATA kwa kupewa vyetu vya kuhitimu. 

Wednesday 13 September 2017

LILIAN LOTH KUIWAKILISHA TANZANIA MASHINDANO YA MISS AFRICA CONTINENTAL 2016/2O17



Katibu mtendaji wa Baraza La Sanaa La Taifa (BASATA) Bw.Godifrey Mngereza (aliyevaa miwani) akimkabidhi bendera ya Tanzania mshiriki wa mashindano ya Miss Africa Continental (Lilian Loth) yanayo tarajiwa kufanyika nchini Afrika ya kusini (Johannesburg). Makabidhiano hayo yalifanyika ofisini kwake Jijini Dar Es salaam.



Mwanadada  Lilian Loth Lazaro mshindi wa  mashindano ya Miss Tanzania Continental 2016/2017 amekabidhiwa rasmi bendera ili kuiwakilisha Tanzania katika mashindano ya Miss Africa continental yanayotarajiwa kufanyika  Afrika ya kusini (johannesberg) mwaka huu. Makabidhiano hayo yalifanyika katika ofisi ya katibu mtendaji wa Baraza La Sanaa La Taifa(BASATA) 22/08/2017.


Lilian Loth alikabidhiwa bendera hiyo baada ya kushinda mashindano ya Miss Tanzania Continental yanayofanyika kila mwaka yakiwa na lengo la kutafuta mshindi atakaye iwakilisha Tanzania katika mashindano ya Miss Africa continental. Mashindano hayo hujumuisha washindi mbali mabali wanao wakilisha nchi zao, yaani kila nchi hutoa mshindi mmoja ili ashiriki mashindano hayo na mwisho kumpata mmoja atakaye wakilisha Afrika katika mashindano ya Dunia.


Mashindao hayo yalianzishwa tokea mwaka 2014,  na hii imekuwa mara ya kwanza Tanzania kutoa mshiriki katika mashindao haya. Mashindano haya huusisha mwaafrika yeyote mwenye vigezo vya kutosha kuitambulisha vyema Afrika katika kueneza utamaduni, mila na desturi za kiafrika.

Mwanadada Lilian Loth Lazaro mwenye umri wa miaka 22 akitokea chuo kikuu cha kampala university anayesoma shahada ya utawala amekuwa mshiriki wa kwanza kushiriki mashindano haya hapa nchini baada ya kushinda mashindano ya Miss Tanzania Continental yaliyofanyika mwaka huu hapa Tanzania.


Aidha katibu mtendaji wa Baraza La Sanaa La Taifa (BASATA) Bw.Godifrey Mngereza alimkabidhi bendera hiyo na kumtaka aiwakilishe vyema Tanzania katika mashindano hayo na alisema ‘nenda ukaiwakilishe  vizuri Tanzania na sisi watanzania tupo nyuma yako na Mungu akubariki’

Mshiriki wa mashindano ya Miss Africa Continental Lilian Loth akiwa na Katibu mtendaji wa Baraza La Sanaa La Taifa Bw. Godifrey Mngereza mara baada ya kukabidhiwa rasmi bendera ya Tanzania ili kuiwakilisha Tanzania katika mashindano hayo Afrika kusini mwaka huu.



Tuesday 12 September 2017

WASANII JIUNGENI NA MFUKO WA HIFADHI YA JAMII.


Bw. Magira Werema (Afisa mikopo kutoka mfuko wa hifadhi ya  jamii (PSPF) akitoa elimu juu ya kujiunga na PSPF kwa wasanii katika viwanja vya Baraza La Sanaa La Taifa (BASATA) alipokuwa kwenye Jukwaa la Sanaa



"Wasanii wengi hapa nchini bado hawajajiunga na mifuko ya hifadhi ya jamii", hayo yalisemwa  na  Bw. Magira Werema (Afisa Mikopo kutoka  Mfuko wa hifadhi ya jamii PSPF)  tarehe 21 Agosti 2017 alipokuwa  kwenye Jukwaa la Sanaa katika viwanja vya Baraza La Sanaa La Taifa (BASATA) ambapo jumla ya wadau  wapatao  sabini (70) walihudhuria programu  hiyo.

Bw. Magira Werema  Afisa mikopo kutoka mfuko wa hifadhi ya jamii (PSPF) aliwataka  wasanii  kujiunga na mfuko wa PSPF ili waweze kunufaika na huduma zinazotolewa na mfuko huo kwani  PSPF wamelenga kusaidia katika majanga  yasiyo kingika kama Magonjwa, Ajari pamoja na Ulemavu. Bw. Werema alisema  “wasanii wengi wanahangaika hasa wanapopatwa na magonjwa hali ambayo huwalazimu kuomba msaada kutoka serikalini
au kuchangishana wao kwa wao ili waweze kupata matibabu”  ilikuondokana na usumbufu huo akawaomba  wasanii wajiunge na PSPF.
Bali na hayo, pia Bw. Magira alieleza mafao mbalimbali yanayotolewa na PSPF mafao hayo ni Fao la Elimu na Ujasilia mali, Mafao ya bima ya afya, Fao la uzeeni, Mikopo ya nyumba pamoja  na viwanja, pia  fao la ulemavu linatolewa, hivyo basi wanachama wake wananufaika na mafao hayo.

Hivyo basi aliwataka wasanii wajiunge  na PSPF ili wanufaike na mafao hayo, kwani wasanii wengi wanahangaika hasa baada ya kuzeeka na hii husababishwa na ukweli kuwa, muziki una muda wake na hufikia kipindi cha kupumzika hivyo basi wakiwa na PSPF wanaweza kupatiwa fao la uzeeni na kuwasaidia kama wasitaafu wengine wanavyo nufaika na mafao ya uzeeni.     
  
Katika Jukwaa hilo, Bw. Augustino Makame kutoka  Baraza La Sanaa La Taifa (BASATA) alitowa ombi kwa PSPF kutafuta namna ya kuwafikia wasanii  hasa waliopo mikoani kwani PSPF haipo kwa  ajiri ya wasanii wa Dar es  salaam tu, pia aliomba PSPF  wawatumie wasanii katika kazi zao hasa wanapokuwa wanahamasisha watu kujiunga na mfuko huo   na wafanyapo mikutano ili kuwainua wasanii.













Na mwisho Bw. Magira alitowa wito kwa wasanii kujiunga na PSPF kwani wakati ni sasa na haina haja kubaki wakihangaika, na alisema hakuna gharama ya kujiunga na mfuko huo, wadau pamoja nawasanii waliokuwepo kwenye Jukwaa hilo waliitikia wito huo kwakuchukua fomu za kujiunga na mfukohuo kwa wingi,  kwani elimuiliyotolewa ilionekana kuwahamasisha kujiunga na mfuko huo.
Bw.Magira Werema (afisa mikopo kutoka PSPF) akijibu maswali mbalimbali kutoka kwa wadau ikiwa ni pamoja na kuelekeza hatua za kujiunga na mfuko huo, ambapo alisema hakuna ghalama yoyote ile inayotozwa ili kujiunga na PSPF
Bw. Magira Werema mwenye suti nyeusi akiwa na Bw. Augustino Makame kutoka ( BASATA) wakijaribu kuchambua changamoto mbalimbali kutoka kwa wadau waliokuwepo kwenye Jukwaa hilo.
Mmoja wa wadau wa sanaa aliyekuwepo kwenye Jukwaa hilo akiuliza swali kwa muwezeshaji hasa juu ya faida  za kujiunga na mfuko wa hifadhi ya jamii PSPF  na hatutua za kujiunga na mfuko huo.

Wadau mbalimbali wa sanaa wakifuatilia kwa makini hoja mbalimbali zilizokuwa zikitolewa katika mkutano huo.