Monday 17 July 2017

TANZIA


Tarehe: 17/07/2017


BASATA Arts Centre                                                             Tel. 2863748/2860485
                                                                                                              
Ilala Sharif Shamba                                                                                                                                                                       
P.O. Box. 4779, Dar es Salaam
E-mail: info@basata.go.tz

YAH: SALAAM ZA RAMBIRAMBI

Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) limepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za msiba wa mke wa Mhe. Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dr. Harrison Mwakyembe Bi. Linah George Mwakyembe aliyefariki dunia usiku wa kuamkia jana katika Hospital ya Aga Khan, jijini Dar es Salaam. 

Baraza limestushwa na kuhuzunishwa sana kutokana na taarifa ya kifo hiki cha Bi. Linah George Mwakyembe ambaye ukarimu wake hautosahaulika kamwe kwa familia yake lakini pia hata kwa wageni wote ambao walibahatika kufika nyumbani kwa Waziri Mhe. Dr. Harrison Mwakyembe.

Baraza linatoa pole kwa Mhe. Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo pamoja na familia yote ya marehemu, pia linawatakia moyo wa subira katika wakati huu wa majonzi ya kuondokewa na mpendwa wetu. 

Baraza liko pamoja na familia ya marehemu katika kipindi hiki kigumu cha majonzi. Mwenyezi Mungu aipumzishe mahala pema peponi roho ya marehemu. Amin.


Godfrey L. Mngereza
KATIBU MTENDAJI, BASATA

No comments:

Post a Comment