Wednesday 26 July 2017

WASANII WAASWA KUONGEZA THAMANI KATIKA KAZI ZAO

Mkurugenzi wa kituo cha Utangazaji cha Clouds Bw. Ruge Mutahaba (katikati), kulia ni Mkurugenzi wa Utawala na Fedha wa BASATA Bw. Onesmo Kayanda na kulia ni Mhasibu Mkuu wa BASATA Bw. Mrisho Mtumwa.
 Mkurugenzi wa vipindi kutoka kituo cha utangazaji cha Clouds Bwana Ruge Mutahaba jana kwenye Jukwaa la Sanaa linalofanyika BARAZA LA SANAA LA TAIFA (BASATA) ambapo mada ilikuwa ni Mnyororo wa Thamani (value chain) aliwaasa watanzania kupitia wasanii kuongeza thamani katika kazi zao ili waweze kuongeza ubora wa wanachokizalisha. 

Bwana Ruge alisema...
"Unapotengeneza muziki ukakamilika, kabla ya kuweka bei ya mauzo sokoni ni lazima uuongeze thamani kwa kukumbuka gharama ulizotumia kwa kila hatua uliyopitia katika kuandaa kazi husika, mfano lazima ukumbuke gharama ya producer, studio, muda uliotumia, usafiri nk ili uweze kuwalipa ama kujilipa kwanza kabla ya kuseti bei ya mauzo sokoni".

Sehemu ya umati wa watu walioudhuria jukwaa hilo

Sehemu ya umati wa watu walioudhuria jukwaa hilo

Bwana Ruge Mutahaba akifafanua jambo katika Jukwaa hilo

No comments:

Post a Comment