Thursday 26 February 2015

TAARIFA KWA WASANII WOTE NA VYOMBO VYA HABARI.

 Katibu Mkuu wa Wizara ya HabariVijanaUtamaduni na Michezo Bi. Sihaba Nkinga. 


























KATIBU MKUU WA WIZARA YA HABARI, VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO ATAKUTANA NA WASANII WOTE SIKU YA  SIKU YA IJUMAA TAREHE 27/02/2015 KUANZIA SAA 6:00 MCHANA.
ENEO NI NI UWANJA WA TAIFA JIJINI DAR ES SALAAM. ATAKAYEPATA UJUMBE HUU ANAOMBWA AMFAHAMISHE NA MWENZAKE.
SHUKRAN.


Wednesday 18 February 2015

Kutoka Johannesburg South Africa, video mpya ya Madee ft Chege – ‘vuvula’ iko hapa



Ni muunganiko wa wakali wawili Madee na Chege ambao baada ya mashabiki wa muziki kuwasikia kwenye audio moja iliyotayarishwa na Dj Maphorisa kutokea Afrika Kusini, sasa time hii pia wametusogezea video ya single hiyo imefanywa na director Adam Juma.
+++Chanzo: millardayo.com

 

Video ya mkali kutoka Kenya, Rabbit King mwenyewe feat. Rich Mavoko- ‘Njoo’



Rabbit King na Rich Mavoko




Mipaka ya kazi za kisanaa inazidi kupanuka kwa mkali kutoka 255 Bongo Flevani, Rich Mavoko ambaye safari hii moja ya vitu vilivyoonekana sana kwenye ukurasa wake wa Instagram ni PICHAZ akizungumzia ujio wa hii ngoma kutoka Kenya, ambayo Mavoko kapewa collabo.
Wimbo ni wa Rabbit King Kaka unaitwa Njoo’.
Nikimwona roho huskip a beat kama saa, msafi na tattoo ya hearts kwa thigh, pesa unajua kupata, matembezi ya bata, maringo ya tausi…”; hii ni sehemu ya verse kutoka kwa Rabbit mwenyewe.
***chanzo: millardayo.com

 



SALAMU ZA RAMBIRAMBI KWA FAMILIA ZA WANAMUZIKI JOHN KITIME NA DULLY SYKES




Tarehe: 16/02/2015

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

BASATA Arts Centre                                                                            Tel. 2863748/2860485
                                                                                                  Fax: 0255- (022) – 286 0486                                                                                                                         
Ilala Sharif Shamba                                                                                                                                                                       
P.O. Box. 4779, Dar es Salaam

RAMBIRAMBI KWA KIFO CHA MKE WA MWANAMUZIKI JOHN KITIME NA BABA YAKE MSANII DULLY SYKES
Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) limepokea kwa masikitiko na majonzi makubwa kifo cha Mke wa Msanii mkongwe wa muziki wa dansi na Mjumbe wa Bodi ya BASATA Bw. John Kitime kilichotokea mwishoni mwa wiki iliyopita usiku wa kuamkia Ijumaa ya Tarehe 13/02/2014.
Aidha, BASATA linatoa salamu rambirambi kwa kifo cha Baba Mzazi wa Msanii Dully Sykes, Mzee Abby Sykes kilichotokea jana Jumapili ya Tarehe 15/02/2015.
Pamoja na vifo hivi kuacha majonzi na huzuni kwa wanafamilia, ni pigo pia kwenye tasnia ya Sanaa kutokana na ukweli kwamba wote wawili kwa njia moja ama nyingine wamekuwa na mchango katika kuhakikisha tasnia hii inasonga mbele kwa kuwa karibu na wasanii John Kitime na Dully Sykes sawia.
Baraza linatoa pole kwa wadau wote wa Sanaa hususan wasanii na Umoja wa mabloga nchini kwa misiba hii. Ni matumaini ya Baraza kwamba, tutaendelea kuenzi mema yote yaliyotendwa na Marehemu hawa hasa kudumisha upendo na amani katika tasnia yetu.
Bwana ametoa na Bwana ametwaa, Amen
Godfrey Mngereza
KATIBU MTENDAJI