Wednesday 14 December 2016

JUKWAA LA SANAA BASATA PALIKUWA HAPATOSHI LEO



Baraza la Sanaa Taifa (BASATA) limefanya program yake ya Jukwaa la Sanaa kwa wadau wa sanaa na wa kazi za sanaa.


Mada ya leo ilikuwa:
Fursa za Sanaa Kutokana na Mabadiliko ya Teknolojia na Dunia ya Utandawazi .

Mtoa mada:  
Ruge Mutahaba (Mfanyabiashara, mtunzi na mdau wa muziki).


Bw. Mutahaba; Alisema “Sanaa yetu ina mapato mengi kama serikali kupitia BASATA na mamlaka nyingine husika zikiamua kubadili mfumo uliopo na kujikita katika mifumo ya sanaa kwa maana ya kibiashara ili mbali na kukuza vipaji na vipato kwa wasanii mmoja mmoja lakini pia kuongeza pato la taifa”.


Pia amewashauri “Wasaani kutokana na mabadiliko ya teknolojia na dunia ya utandawazi, sanaa ni biashara kubwa kwasasa, hivyo tunapaswa kufahamu na kujua vizuri  kuchanganya vionjo mbalimbali vya utamaduni wetu wa Kitanzania ili kupata ladha inayouzika sokoni hata kimataifa”.


Aidha amewasihi wasanii kuzingatia na kuwa na weledi wa kutosha wa kutumia mitandao ya kijamii ili kuweza kujitangaza kiurahisi na kwa haraka lakini pia kufikisha kazi zao kwa jamii kubwa zaidi.





Ruta Maximilian Bushoke "Bushoke" naye alikuwpo akifatilia mjadala kwa makini kwenye Jukwaa la Sanaa


Mtendaji wa BASATA Bw. Kurwijira Maregesi Ng'oko akitoa ufafanuzi juu ya jambo fulani kwenye Jukwaa hilo.
Katibu Mtendaji wa BASATA Bw. Godfrey L. Mngereza akitoa ufafanuzi wa jambo fulani.









No comments:

Post a Comment